Wednesday, July 20, 2011

Niionavyo njaa ya Pembe ya Afrika {Somalia, Ethiopia, etc}

Wakati ule wa utumwa wa wana wa Israel nchini Misiri Mungu alimsaidia Yusufu kufasiri ndoto ya Farao, ni ndoto hii na fasiri yake sahihi ndizo zilisaidia nchi ya Misiri kuwa taifa lenye nguvu kuliko mengine ya wakati wake {Mwanzo 41}. Baada ya tafsiri ya ndoto ile Farao alimteua Yusufu kuwa mtendaji wake mkuu ili kufanikisha fasiri ya ndoto yake (Farao) na kupitia Yusufu Misiri ilitumia vyema miaka saba ya neema kujikusanyia nafaka ya kuwatosha wao na mataifa ya jirani katika miaka saba ya ukame na dhiki, si tu taifa la Misiri lilipata chakula bali pia liliweza kuwa na nguvu kuliko yote kwa sababu ya utajiri uliotokana na hekima ya Yusufu.
Ninapoyatazama matukio ya Somalia na ukosefu mkubwa wa chakula nayafananisha na ndoto ya mtumwa Yusufu nchini Misiri, njaa ya aina hii haitakuwa ya mwisho, historia inatuambia kuwa angalau kila baada ya miaka kumi kunakuwa na ukosefu mkubwa wa chakula unaotokana na ukame. Kwa kutumia ukweli huu naona hii ni baraka kwani tukiitumia vizuri itakuwa ni fursa ya kutuwezesha kufaidika na ukosefu mkubwa wa chakula wa mwaka 2021 kama ambavyo Misiri iliweza kujikusanyia chakula kwa kipindi cha miaka ile saba ya neema.
Tatizo kubwa la uzalishaji nchini kwetu ni ukosefu wa maji, lakini bahati nzuri ni kwamba mvua hunyesha na mtu akichimba bwawa anauhakika wa kuwa na maji ya kutosha ndani ya miaka mitatu.
Ushauri wangu:
Tuanze sasa kujiandaa na ukame wa 2021 kwa uzalishaji wa chakula cha ziada tukiweka mkazo kwenye kilimo cha umwagiliaji, bahati nyingine nzuri ni kuwa sasa kuna fursa nyingi ambazo zinasubiri kuchukuliwa. Nitatoa mfano wa pesa zinazotarajia kutolewa na wahisani kupitia mradi wa SAGCOT (google neno hili kwa taarifa zaidi). Lakini bila maandalizi sasa fursa hizi zitachukuliwa na wageni na tutaendelea kulalamika bila mambo kubadilika sana.
Kijijini kwetu kuna jamaa alikuwa anachimba malambo kwa ajiri ya kunyweshea mifugo na gharama yake siyo kubwa sana, mimi nitafanya majaribio kwa kuchimba bwawa kutumia mheshimiwa huyu. Lakini kitu kingine ambacho tunaweza kuanza kujiandaa ni kujikusanya ili tuwe na nguvu ya pamoja na tuweze kunufaika na fedha zinazotolewa kupitia madirisha kama hili la SAGCOT ambalo linaweka msisitizo zaidi katika kuwaendeleza wakulima wadogo kupitia vikundi vyao, lakini pia ili umoja una manufaa mengine kuwa uzalisha unapokuwa mkubwa inakuwa rahisi kupata soko na pia kuweza kuongeza thamani kwa urahisi.
Pia msisahau kuchangamkia fursa ya kupata ardhi, nasiki Lindi kuna maeneo mengi ya wazi ambayo tunaweza kuyachangamkia na kujinufaisha kama wawekezaji wa ndani, nitakuwa na safari ya ya kuuelewa mkoa wa Lindi mwezi August nakaribisha kwa yeyote atakayependa tufanye safari hii pamoja

Tuesday, July 19, 2011

Je umekubali kutawaliwa?

Uwezo tunao, sababu tunayo, na nia tunayo

Hii ilikuwa sehemu ya hotuma ya Mwalimu J. K. Nyerere wakati akilihutubia taarifa baada ya Tanzania kuvamiwa na nduli Idd Amini Dadaa wa Uganda mwaka 1978. Kutawaliwa ni fedheha, kutawaliwa maana yake ni kupoteza uhuru na utu wako. Kwa sababu hizi za msingi Taifa la Tanzania liliingia vitani kupambana na hatimaye kumpiga nduli Idd Amin ili kuepuka fedheha na kuhakikisha uhuru wa Tanzania hauingiliwi na mtu yeyote.
Kuwa masikini maana yake ni kuwa mtumwa, kuwa masikini maana yake ni kutawaliwa, ni sawasawa na kuwa chini ya ukoloni. Mababu zetu wakiongozwa na viongozi wao akina Mkwawa, Kijekitile Ngwale, Isike, na wengine wengi walipigana kufa au kupona kupinga kutawaliwa na wakoloni kwa sababu ya fedheha waliyoipata walipokuwa wametawaliwa na wageni. Walikataa kufanyishwa kazi wasizozipenda kwa ujira mdogo ama pasipo ujira wowote, walikataa kufanyishwa kazi kwa mababu zao, walikataa kulipishwa kodi walizotozwa ili ziwasaidie watu wengine, walikataa kudhalilishwa kwa kupigwa vipoko mbele ya watoto na wake au waume zao, walikataa kupoteza heshima yao, walikataa kunyimwa haki zao za msingi kama kusafiri bila kubaguliwa, kusafiri bila vizuizi vya aina yeyote ile, kubaguliwa katika kupatiwa huduma.
Ukiwa masikini utafanyishwa kazi usizozipenda, utafanyishwa kazi kwa ujira mdogo, na utafanyishwa kazi bila ridhaa yako. Kila nikiiona mzee akifanya kazi ya fedheha kama kufagia barabara, ulinzi wakiwa na umri mkubwa naona ukoloni uletwao na umasikini, kila nikiona mtu ameshindwa kupata huduma sitahili za afya kwa sababu ameshindwa kumudu gharama za matibabu najua utumwa uletwao na umasikini ni hatari kuliko maladhi wanayougua. Kila nikiona watoto wameshindwa kupata haki yao ya msingi ya kupumuzika na kucheza kwa kufanyishwa kazi katika umri mdogo ili waweze kupata mahitaji yao, kila nikiona mtoto ameshindwa kupata haki yake ya msingi ya kupata elimu bora anayositahili naona udhalimu na mateso yaletwayo na umasikini, kila nikiona watu wakibebwa kwenye mikokoteni ama malori wakisafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine naona mateso yaletwayo na nduli umasikini. Kila nikiona watu wakikosa mahitaji yao ya mhimu kama malazi, chakula na mavazi wanayostahili naona umasikini ukiwa kazini, naona utumwa ule ule walioukataa mababu zetu, naona ukoloni walioukataa akina Kinjekitile, naona uvamizi alioukataa Mwalimu Nyerere.
Kinjekitile aliweza kuhamasisha majeshi ya mababu zetu kwa kutumia maji, Kinjekitile alijua tatizo kubwa lao lilikuwa liko akilini mwao; akafanikiwa kulitafutia dawa kwa kuwapa maji aliyowaaminisha kuwa yalikuwa na uwezo wa kuzuia risasi za wakoloni. Kinjekitile alifanikiwa kuwahamasisha mababu zetu na kuwatisha Wajerumani waliokuwa na siraha bora na kali zaidi kwa kutumia maji ambayo yalikuwa hayana uwezo wa kuzuia risasi kama walivyoaminishwa. Kilichowatisha Wajerumani ulikuwa ni ujasiri wa watu waliokuwa na siraha duni kuliko zao. Kilichomkimbiza nduli Idd Amin na majeshi yake ilikuwa ni ujasiri na umoja wa majeshi ya Tanzania, baada ya hotuba ile ya Nyerere kila Mtanzania alikuwa tayari kwenda vitani ingawa kila mtu alijua vita havina macho lakini walihamasika kuhakikisha kuwa taifa lao linaondokana na fedheha ya kutawaliwa. Wake kwa waume walijikusanya kumfuata, aliingiwa na hofu alivyouona umma wa Watanzania uko nyuma ya kiongozi wao wakiwa tayari kufa ili mradi wanarudisha heshima ya taifa lao.
Leo hii kuna watu wengi wamezama kwenye dimbwi la umasikini na wameridhika kuwa hawawezi kuondokana na umasikini kwa sababu hawana nyenzo, hawana siraha. Wengi, wakiwemo viongozi wa taifa letu wanadhani kuwa umasikini huo utaondolewa na watu wengine kwa kuwaonea huruma. Wengi wanajua hawawezi kuondoka kwenye bonde hilo kwa sababu ama hawana mitaji, ama hawana elimu, ama kitu kingine chochote ambacho wanadhani wakikipata wataondoka pale walipo. Historia inatuambia kuwa hili halitawezekana na halitatokea hadi pale wao wenyewe watakapokata shauri ya kuondoka kwenye kituo chao, cha umasikini na maisha duni. Ushindi wa vita yoyote huanzia akilini mwa mpiganaji, huanza pale jemedari na majeshi yake watakapoamua kuwa ni ushindi pekee ndio utawapa mapumuziko, tofauti na hapo adui atashambuliwa na kukoseshwa usingizi mpaka atakapo salimu amri. Mitaji na elimu ni vitendea kazi tu ambavyo hurahisha kazi vinapokuwepo lakini siyo sababu ya kufanikiwa.
Ndugu msomaji wangu, ni pale tu utakapo amua kuwa umasikini basi, ni pale tu utakapochukia kero na fedheha zote ziletwazo na umasikini na kuamua kuwa lazima uondokane na fedheha hizo ndipo utakoweza kuondokana na umasikini au hali duni ya maisha yako. Sitaweza, na sina uwezo wa kukueleza ni namna gani utaweza kuondoka pale ulipo kwa sababu kila mtu ana malaika wake, na kila mtu ana kipaji chake kilicho tofauti na watu wengine. Unaweza kuondokana kwa kubadilisha kazi kama utatafakali na kuona kuwa kwa namna unavyofanya si rahisi kuondokana na hali yako duni, unaweza kuendelea kufanya kazi yako ile ile lakini ukabadilisha namna unavyoifanya na namna unavyoyatumia mafao yanayotokana na kazi yako. Katika dunia hii kuna watu wamekuwa mamilionea kwa kufanya kazi unayoidharau, kuna ambao wametajirika kwa kuzoa taka, ndiyo, kuzoa taka! Kuna wengine wengi wametajirika kwa kupika, wapo pia wengi waliotajirika kwa kilimo. Kinachowatoutisha waliofanikiwa na wale ambao wameshindwa ni namna wanavyofikiri, kama ukiamua kuondokana na umasikini kwa kutumia kilimo lazima ukipende kilimo na ujiaminishe kuwa hakuna kitu kingine kitakutoa hapo isipokuwa kilimo, kama umeamua kuwa utaondokana na umasikini kwa kuokota taka lazima uzipende taka na kila unapoziona ufurahi kuwa ile ni fursa yako ya kuondokana na umasikini na siyo uchafu! Kama unataka kuondokana na umasikini ukiwa mwalimu lazima kwanza ukate shauri na kuamini kuwa ni kuwatoa watu ujinga pekee ndiko kutakako kutoa kwenye lindi la umasikini, ni lazima ufurahi kuona mtu hafahamu kitu unachokifundisha siyo kwa sababu hajui bali ni kwa sababu hiyo ni fursa yako kuondokana na umasikini, ukiwaona wanafunzi wako na mazingira ya kazi yako kuwa ni kero hautaweza hata siku moja kufanikiwa ukiwa mwalimu, ni lazima kwanza uione kazi yako kuwa ni fursa ya wewe kufanikiwa. SIRI YA USHINDI NI MOJA, KUTOPUMUZIKA HADI USHINDI UMEPATIKANA.

Saturday, July 9, 2011

Poverty is evil!

“The greatest of evils and the worst of crimes is poverty... our first duty – a duty to which every other consideration should be sacrificed—is not to be poor.” George Barnard Shaw

Every time I walk in the street and see poor people I think about it and say to myself I could as well be this poor if I were to be sacked from job and remain unemployed for six months, every time I see men and women working in the old age I reflect it on me that I could wind up just like them, when I think of the beautiful dreams of my vacations in resort islands I realize that they could remain just dreams unless I do something different.

Have you asked yourself these and other similar questions, what are your answers. Let us share them here and see how we could work together to realize our beautiful dreams. The dreams of our young ones attending the best universities there is, the dreams of our beautiful homes becoming reality, the dreams of buying the best luxuries for our loved one.... let us dream on and work to realize these dreams... IT IS POSSIBLE IF WE DARE TRY WHAT WE DAY DREAM... there is no short cuts, the only way that we can tell whether our dreams can be realized is by trying!